KOCHA Mkuu wa Yanga, Hans Van Der Pluijm jana amewaongoza mamia ya mashabiki wa timu hiyo wilayani Muheza mkoani Tanga kufungua tawi jipya. Tawi hilo limefunguliwa eneo la Majengo-Shimoni wilayani humo wakati timu hiyo ikielekea Tanga mjini kwa ajili ya mpambano wao dhidi ya Coastal Union utakaopigwa Uwanja wa Mkwakwani hapo kesho.
Post a Comment